Thursday, August 18, 2016

MARINATION YA NYAMA YA KUCHOMA


MAHITAJI
Nyama 1 kg, Buttermilk 250 mls (waweza kutumia mtindi), limao 1, tangawizi (grated) vijiko 2, them vijiko 2, pilipilimanga kijiko cha chai 1, curry powder kijiko 1, garam masala kijiko 1 na turmeric powder kijiko 1 (ukiweza kupata fresh ni bora zaidi ikwangue (grate) kama tangawizi, mafuta ya kupikia kijiko 1 (natumia Olive oil), chumvi kiasi upendacho.

JINSI YA KUANDAA
Changanya vitu vote kwenye bakuli isipokuwa chumvi na limao  Mchanganyiko ukiwa tayari weka nyama changanyanya vizuri kisha kamulia limao, weka chumvi changanya tena. Weka nyama kwenye mfuko wa plastic funga vizuri weka kwenye friji masaa 2 mpaka 6 (inategemea unataka kuchoma saa ngapi). Ukiwa tayari choma, tengeneza kachumbari ya kiswahili (nyanya, kitunguu, ndimu, na chumvi), Enjoy!!!

4 comments: