Thursday, August 4, 2016

ANDAZI LA NGANO ISIYOKOBOLEWA



ANDAZI LA NGANO ISIYOKOBOLEWA

MAHITAJI 

*Ngano 500g *Mayai 2 (yapige mpaka povu) *Baking powder (CHAPA MANDASHI nzuri zaidi) kijiko cha chakula 1 *Hamira kijiko cha chakula 1 *Mafuta ya kula vijiko vya chakula 2 *Iliki (ukipenda) kijiko cha chakula 1 (weka zile punje nyeusi kwenye sufuria kavu jikoni geuzageuza kama dakika 1 kisha twangwa zikiwa fresh, sipendi ile ya unga). *Sukari kiasi upendacho *Maziwa fresh ya baridi ya kukandia


JINSI YA KUANDAA 

WEKA UNGA NA VITU VYOTE VIKAVU KWENYE BAKULI CHANGANYA VIZURI. WEKA MAYAI KANDA. WEKA MAFUTA YA KULA KANDA. ANZA KUWEKA MAZIWA TARATIBU HUKU UNAKANDA MPAKA UPATE LILE DONGE UNALOHITAJI. ANGALIZO: UNGA WA MAANDAZI UWE MGUMU KIASI KULIKO WA CHAPATI AU SKONZI MAANA UKIUMUKA UNALEGEA ZAIDI HIVYO MAANDAZI YATANYONYA MAFUTA UKICHOMA. UKIMALIZA KUKANDA (BAADA YA DAKIKA KAMA 10, FUNIKA DONGE LAKO NA KITAULO KISAFI ACHA KAMA NUSU SAA, KANDA TENA KWA DAKIKA 5 KISHA FUNIKA TENA ACHA UUMUKE UWE MARA 2. KATA UMBO UPENDALO, CHOMA.

5 comments:

  1. Bi Moremi, asante sana kwa maelekezo yako. Ingawa nina swali, hivi kuna tofauti nisipotumia maziwa?

    ReplyDelete
  2. Bi Moremi, asante sana kwa maelekezo yako. Ingawa nina swali, hivi kuna tofauti nisipotumia maziwa?

    ReplyDelete
  3. Wewe ni noma aisee nimekushindwa
    Big up sana

    ReplyDelete
  4. Ngano nkinunua nakusaga mwenyew itafaa maana sehem nyingine kupata unga huu ni shida na cjawah kuuona dukan

    ReplyDelete
  5. Ngano nkinunua nakusaga mwenyew itafaa maana sehem nyingine kupata unga huu ni shida na cjawah kuuona dukan

    ReplyDelete